Pages

Friday 19 July 2013

NYS Ni LAZIMA!!! Vijana kujiunga baada ya KCPE

Bunge la senet limepitisha mswada utakaopelekea vijana wanaomaliza shule za upili nchini kujiunga na huduma ya vijana NYS kabla ya kujiunga na vyuo vikuu au vyuo vingine vya mafunzo.


Hatua hiyo imechukuliwa ili kuwezesha vijana kupata mafunzo ya taaluma tofauti na kupalilia uzalendo kabla ya kujiunga na masomo ya vyuo vikuu au shughuli zozote baada ya kumaliza shule za upili.





Haya ni marudio ya hali ilivyokuwa hadi 1989 ambapo walioteuliwa kujiunga na vyuo vikuu kwanza walipata mafunzo ya miezi mitatu katika NYS.

Seneti ilipitisha kwa kauli moja hoja hiyo iliyowasilishwa na seneta maalum, Beatrice Elachi aliyetaka wanaomaliza masomo ya shule za sekondari wasaidiwe kujiunga na NYS ili wapate mafunzo muhimu.

Katika hoja yake, Elachi ambaye pia ni kiranja wa walio wengi katika seneti, anataka wanaohitimu baada ya kupata mafunzo kutoka NYS, wapatiwe nafasi ya kwanza ya ajira katika serikali za kaunti na serikali kuu.

Maseneta wamesema kufanya hivyo kutawasaidia vijana wa nchi hii waafikie haki zao za kiuchumi na kijamii.

No comments:

Post a Comment